Tuesday, March 22, 2016

Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete awasili Tunisia kusuluhisha mgogoro wa Libya


Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Mwakilishi Maalum wa Umoja wa Afrika wa Usuluhishi wa Mgogoro wa Libya, amewasili jana Jijini Tunis nchini Tunisia  kushiriki Mkutano wa 8 wa Nchi majirani wa Libya.

Mkutano huo umeitishwa na Serikali ya Tunisia, na ni muendelezo wa jitihada za nchi majirani kusaidia kuleta hali ya amani na usalama nchini Libya.

Rais Mstaafu Kikwete amewasili Tunis akitokea Salalah nchini Oman alikoshiriki Mkutano wa Kamati ya Bunge la Kuandika Katiba ya Libya.

Akiwa Jijini Tunis, Jana tarehe 22 Machi, 2016 Dkt. Kikwete amefanya mazungumzo na Waziri wa Masuala ya Maghreb, nchi za Kiarabu na Afrika, wa Algeria Mheshimiwa Abdelkader Messaleh, aliyemtembelea hotelini kwake.

Katika mazungumzo hayo, Waziri Messaleh amempongeza  Rais Mstaafu Kikwete kwa kuteuliwa na Wakuu wa Nchi wa Umoja wa Afrika kusuluhisha mgogoro wa Libya. Amemueleza hali ya usalama na kisiasa ya  Libya na mtizamo wa nchi yake juu ya namna bora ya utatuzi wa mgogoro huo, na akamhakikishia ushirikiano wa Serikali ya Algeria katika jukumu lake alilokabidhiwa na Umoja wa Afrika.

Kwa upande wake, Rais Mstaafu Kikwete amemshukuru Waziri Abdelkader Messaleh kwa maelezo yake na ushirikiano aliomuahidi na akamueleza matumaini yake ya kupatikana kwa suluhu ya mgogoro huo hasa ikizingatiwa kuwa nchi jirani na Libya na Umoja wa Afrika zitashirikiana na wadau wote kuhakikisha mgogoro huo unatatuliwa.

Rais Mstaafu Kikwete amesisitiza kuwa suluhisho la kudumu la mgogoro wa Libya liko mikononi mwa wananchi wa Libya wenyewe.

Katika ziara yake nchini Tunisia, mbali na kuhudhuria Mkutano wa 8 wa nchi jirani na Libya,  Rais Mstaafu Kikwete anatarajiwa pia kukutana na Waziri Mkuu Mteule na Mwenyekiti wa Baraza la Utawala la Libya,  (Presidency Council) Mheshimiwa Fayez Al-Sarraj,  wadau wengine wa Libya  pamoja na kutembelea Ofisi ya Ujumbe wa Umoja wa Afrika kwa Libya iliyoko jijini Tunis.

Rais Mstaafu Jakaya Kikwete anatarajiwa kurejea nchini tarehe 25 Machi, 2016.

Imetolewa;
Ofisi ya Rais Mstaafu.
Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete
Tunis
22 Machi, 2016
Rais Mstaafu wa awamu ya nne na Mwakilishi Maalum wa Umoja wa Afrika katika Mgogoro wa Libya Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, akizungumza na Waziri wa Manghreb, nchi za Kiarabu na Afrika wa Aljeria Mheshimiwa Abdelkader Messaleh, aliyemtembelea hotelini kwake katika Jiji la Tunis, Nchini Tunisia.
Share:

Saturday, November 16, 2013

PICHA: Hii Ndio TV inayouzwa milioni 75




Niliwahi kuuliza kwa watu wa nguvu shilingi milioni 75 wakipata watatumia kwenye nini?, majibu ya wengi yalikua ni kujenga nyumba na kununua gari huku wengine wakisema watawekeza kwenye biashara.
Sasa basi, pamoja na hiyo milioni 75 kuonekana inaweza kufikiriwa kufanya mambo hayo makubwa ya kimaisha… imefahamika kiwango hicho cha pesa kinaweza kuishia kwenye kununua TV moja tu hii mpya ya Samsung ya inch 85 na usirudishiwe chenchi.
tovuti hii ilipotembelea duka lao Mlimani City, imeambiwa TV hii ina vitu vingi vya kipekee ikiwemo kutumia ishara ya mkono, sauti, na sura kufanya setting mbalimbali ikiwemo kupunguza sauti badala ya kutumia remote.104 
Smart contents mfano Instagram, twitter, facebook na apps nyingine mbalimbali ambapo unaweza kutumia Internet kuwasiliana kwenye mitandao mbalimbali kama vile skype ambapo mnaweza kuonana zaidi ya watu watatu kwa wakati mmoja.
Ina music system yenye mziki mzito hapohapo hivyo ukiwa nayo huna haja ya kununua home theatre, pia faster speed squad core processor.
Digital tuner unaweza kupata local free channels zaidi ya 40 bila decorder na ukitaka channel za kulipia utatumia smart card ambayo unaiweka kwenye smart card slot nyuma ya TV yako.
Vilevile ukiwa na samsung smart phone unaweza kuiunganisha na TV ukaplay videos, music video games kutoka kwenye simu yako.
105
102
101

Source: Millard Ayo
Share:

"Mhe. Kapuya hana kosa la kujibu kabisa"...KOVA

Shaggy Sadick mwenye umri wa miaka 18, mkazi wa Musoma mjini.
Akizungumza kwa masikitiko makubwa, dada wa Shaggy, Mariam Sadick, alisema mdogo wake alianza kuumwa ugonjwa huo tokea akiwa na umri wa miaka 12 na kwa muda wote huo, wamehangaika katika hospitali mbalimbali nchini bila mafanikio.
Alisema awali walianza kumpeleka katika Hospitali ya Musoma na baadaye Bugando jijini Mwanza ambako baada ya vipimo, iligundulika kwamba alikuwa akisumbuliwa na tatizo la moyo ambao umejaa maji, ugonjwa ambao anapaswa kutibiwa nje ya nchi ili kuumaliza.

“Kwa kweli tumehangaika naye sana kumsaidia apone, lakini imeshindikana kwani ili apone, wanapaswa kumpeleka nje ya nchi kwa matibabu, kitu kinachotishia uhai wake kwani familia ni duni,” alisema dada huyo.
Dada huyo alizidi kulia kwa kusema kwamba kingine kinachomsikitisha ni kwamba mdogo wake amekosa kufanya mtihani wa kidato cha nne mwaka huu kwani kwa matatizo aliyonayo, hawezi kutembea tumbo limefika hadi magotini.
Alisema wakati wa kulala ukifika, mdogo wake hupata wakati mgumu kwani wanalazimika kumuwekea mito mingi ya kulalia nyuma yake, vinginevyo anaweza kupoteza maisha kwa sababu ya kushindwa kupumua vizuri.
Kwa kweli kitu ambacho kinatusikitisha wote ni kukosa kufanya mtihani wa kidato cha nne, maana hawezi kutembea tena  wakati wa kulala ndiyo kama hivyo,” alisema.
 Mtoto Shaggy yupo katika mateso makali sana, anahitaji msaada wa hali na mali ili aweze kuyaokoa maisha yake ili apate matibabu, endapo utaguswa na habari yake, wasiliana na chumba cha habari kwa namba  0713 612 533.
Share:

Changudoa akiri kuwa amechoshwa na utumwa wa Ngono..!

INAWEZEKANA umeshalizwa na mengi, umesikitishwa na vingi lakini stori ya dada Aziza Athumani (21), anayefanya biashara ya kuuza mwili wake, inatia uchungu sana
Aziza anayefanya biashara ya kujiuza jijini Dar es Salaam kwa sasa ni mgonjwa lakini analazimika kuendelea na biashara hiyo ili aweze kujikimu.

Sasa, hebu fuatilia mahojiano yetu na Aziza.
Ijumaa: Hebu tuambie...ni nini hasa kilikusukuma kuingia kwenye biashara hii haramu?
Aziza: Maisha kaka yangu, maisha. Nilizaliwa Mtwara miaka 21 iliyopita. Niliishi na mama na wadogo zangu. Baba yangu anaishi hapa Dar. Bahati mbaya,  baadaye mama alifariki dunia. Hapo ndipo maisha yalipoanza kuwa magumu.
Ijumaa: Kwa hiyo shughuli ya kujiuza ulianza hukohuko Mtwara?
Aziza: Hapana. Maisha yalivyokuwa magumu baada ya mama kufariki, niliamua kuja Dar kutafuta maisha. Nilifikia kwenye baa moja iliyopo Sinza, nakumbuka ilikuwa mwaka 2010, nikiwa na miaka 17. Kipato kilikuwa kidogo sana lakini wateja walikuwa wakiniachia chenji ndogondogo.
Ijumaa: Kwa siku ulikuwa unaweza kuingiza shilingi ngapi?
Aziza: Hadi 10,000 nilikuwa nafikisha, wakati mwingine inazidi kidogo. Tatizo wanaume wa baa siyo wastaarabu. Wakilewa wanaanza kukushikashika. Mimi nilikuwa mdogo kwa hiyo nilivyokataa, nilifokewa na meneja. Nikawa nawaachia.
Siku moja, mteja mmoja akanitaka, nikakataa. Ikawa kama wameambiana. Karibu wote waliokuwa wakiniachia chenji wakanitongoza, wote nikawakataa, kuanzia hapo wakawa hawaniachii chenji tena. Maisha yakabadilika.
Ijumaa: Yakawaje?
Aziza: Nikawa sina fedha za kutosha kujikimu mimi na wadogo zangu. Wakati mwingine nilikuwa nalala mwenyewe geto (chumbani), wenzangu wote waliondoka na wateja (kulala nao kwa kujiuza). Nikiwaomba pesa, wananicheka, wakaniambia na mimi nitoke. Nikajaribu...kumbe nilikuwa naingia kwenye moto (analia)...nikajikuta nimezoea mchezo wa kujiuza.
Ijumaa: Usilie tafadhali, tulia. Baada ya hapo ikawaje sasa?
Aziza: Niliona biashara ya kujiuza inalipa zaidi kwa hiyo nikaamua kuachana na baa na kujikita moja kwa moja kwenye uchangudoa. Siamini kama mimi ni changudoa lakini sitaki kabisa hii kazi, ni shida tu kaka.
Ijumaa: Pole sana...vipi kuhusu baba yako? Halafu huo mguu una tatizo gani? Pia unaweza kueleza kidogo kuhusu elimu yako?
Aziza: (analia sana – zilipita dakika tano akiendelea kulia. Juhudi za kumbembeleza zilizaa matunda baada ya muda huo).
Ijumaa: Najua inauma sana. Jipe moyo. Unaweza kuendelea sasa!
Aziza: (anafuta machozi) Huyo baba...mzee Athumani ndiyo chanzo cha matatizo haya yote! Mimi sijasoma, niliishia darasa la saba tu. Lakini nikasema nitajitahidi angalau niwasomeshe wadogo zangu ndiyo maana nikaja mjini na kujikuta nimeishia kwenye biashara ya kujiuza.
Kuna tukio ambalo siwezi kulisahau. Ilikuwa Jumamosi, saa 9 usiku, mwezi wa saba, mwaka 2011. Mimi na rafiki yangu Asha tulikuwa tumetoka kujiuza Kinondoni. Tulikodisha pikipiki moja, tukapanda kwa mtindo wa mshikaki. Kwa bahati mbaya, tulipofika Magomeni tukapata ajali mbaya. Asha na dereva walikufa palepale...Mungu amrehemu rafiki yangu Asha (analia tena...).
Nikapelekwa Muhimbili, Kitengo cha Mifupa (MOI), nikalazwa kwa siku kadhaa. Mguu wangu ulikuwa umeharibika sana na hivi unavyoona nina vyuma. Niliporuhusiwa hospitalini, nikaenda kwa baba yangu mzee Athumani, Tandika. Cha ajabu, aliponiona nina magongo, akanifukuza akisema, eti mimi siyo mwanaye. Nililia sana, lakini kwa sababu nilikuwa na akiba kidogo nikaamua kurudi nyumbani kwangu Tandale nilipopanga chumba kimoja.
Pesa ilivyoisha, nikalazimika kurudi tena mtaani kujiuza na hii hali yangu ya magongo. Maisha haya! Sijui kwa nini inakuwa hivi jamani!
Ijumaa: Pole sana dada. Hebu tuambie...unakutana na changamoto gani katika kazi yako?
Aziza: Nyingi lakini kubwa ambayo sitaweza kuisahau ni kubakwa na wanaume watatu kwa mpigo, tena nikiwa na magongo yangu. Iliniuma sana. Wanadamu wana roho mbaya sana. Nilikutana na kaka mmoja, tukakubaliana angenipa shilingi 5,000 kwa muda mfupi.
Akasema, hana pesa ya kwenda gesti hivyo tukaenda kwenye Uwanja wa Urafiki, Shekilango. Nikashangaa nimekutana na wenzake wawili, nilipokataa, walinitolea kisu, ikabidi nikubali tu. Niliumia sana siku hiyo (analia – waandishi wanambembeleza).
Tukio lingine ni pale nilipokutana na mwanaume mmoja mwenye asili ya India, akanidanganya na kuniambia nimzalie mtoto, nikabeba mimba yake. Akanikana.
Huwezi amini kaka zangu, hapa nina mtoto mdogo, hata miaka miwili hajafikisha na nilianza kutoka na kuendelea kujiuza, mtoto akiwa na miezi mitatu tu. Mungu anamnusuru mwanangu, anaendelea vizuri.
Ijumaa: Kwahiyo kwa sasa unafikiri nini juu ya changamoto hizi za maisha yako? Bado unaendelea na shughuli hii?
Aziza: Uongo dhambi kaka, bado najiuza lakini nikipata mtaji wa biashara na matibabu nitaacha. Natakiwa kurudi tena MOI mwezi wa pili mwakani kwa ajili ya kuondolewa vyuma, nimeambiwa niende na laki tatu.
Kama umeguswa na kisa cha Aziza na unataka kumsaidia kwa hali na mali, wasiliana naye moja kwa moja kwa namba 0714 021105.

-Gazeti la ijumaa
Share:

BAADA YA FILAMU ZAO KUBUMA SOKONI...BONGO MUVI SASA WASHIKANA UCHAWI...!!

Tuhuma ya mastaa Bongo kujihusisha na mambo ya ulozi au uchawi imeibuliwa upya na safari hii bundi kajikita zaidi kwenye kiwanda cha sinema za Kibongo, Ijumaa lina ripoti kamili.

http://4.bp.blogspot.com/-6rq5Op4EJJk/TvHoS15grOI/AAAAAAAACVA/0DnQiFtM1BY/s1600/26.jpg
UCHUNGUZI
Uchunguzi wa gazeti hili ndani ya ulimwengu wa mastaa hao ulibaini kwamba, ukiwaacha wale wa Bongo Fleva ambao wamekuwa wakishikana uchawi kila kukicha, kwenye filamu ndiko hakufai.

Ilibumburuka kwamba masuala ya kurogana ndiyo yamesababisha filamu za baadhi yao kudoda na kukosa soko.
Inaelezwa kwamba mbali na sinema  zao kubuma sokoni pia wamekuwa wakizibiana riziki za tenda kama ilivyokuwa zamani.

Elizabeth Michael 'Lulu'.
KIVIPI?
Kwa mujibu wa ‘mtaalam’ wao mwenye kituo cha kazi huko Yombo-Buza, Dar, wanachokifanya ni kufifisha na kuzimana nyota hivyo kumpotezea mhusika mvuto kwenye jamii.
“Unajua kuna mastaa ambao walikuwa na majina makubwa sana lakini siku hizi siyo kama zamani.

“Baadhi wanawaroga wenzao kwa kuwasababishia matatizo ya magonjwa au kwenye familia,” alisema mmoja wa wasanii waliokuwa waking’ara zamani lakini siku hizi kafifia huku akimtolea mfano mwigizaji mmoja wa kiume ambaye mkewe aliwahi kumkuta na hirizi.
Katika uchunguzi huo, baadhi ya mastaa walikuwa wakinyoosheana vidole wao kwa wao huku listi ndefu ya mastaa wanaokesha kwa waganga kuwamaliza wenzao ikianikwa (majina tunayo).
Ili kupata uthibitisho wa uchunguzi huo, gazeti hili lilizungumza na baadhi ya vinara wa filamu za Kibongo ambapo wengi walikiri kukithiri kwa ushirikina kwenye tasnia hiyo.

JACOB STEVEN ‘JB’: Sanaa yoyote ili idumu muda mrefu inahitaji baraka na neema ya Mungu. Sisi tulianza enzi za Nyota Ensemble ‘Mambo Hayo’, baadaye ilikuja Kaole Sanaa Group ndipo kukaibuka mapinduzi sisi tukashuka.
Mimi siamini mambo ya uchawi ila naamini katika kazi tu, wasanii waache kufanya kazi kimazoea.

Masuala ya kurogana mimi spendi kuyapa nafasi maana hayo kila sehemu yapo, ninachoweza kusema ni kwamba wasanii wengi wa Bongo hawapo ‘siriasi’. JACQUELINE WOLPER: Mimi naamini sana katika kazi lakini kwa kuwa Mungu ndiye kanipa jina hili, sina budi kumshukuru yeye ila kama nimelipata kwa njia ya uganga basi nikose kabisa.
ROSE NDAUKA: Uchawi ni ishu inayonisikitisha sana na ukweli wapo mastaa wanafanya mambo hayo ili wapande. Mimi najua Mungu hawezi kuwasaidia so nawashauri wafanye kazi, wasihangaike na uchawi kwa sababu hauwezi kuwapandisha.
KAJALA MASANJA: Kusema kweli uchawi unatajwa sana kwenye tasnia ya filamu Bongo hadi inanifanya kuamini hivyo kwa sababu kuna watu kweli wakikuona unang’ara kwenye muvi watafanya kila wawezavyo ili wakushushe tu na hasa kwa njia ya ushirikina.
SINGLE MTAMBALIKE ‘RICHIE’: Mimi asili yangu ni Mwanza so kama ujuavyo watu wa Mwanza ni wachapa kazi, so nipo makini sana na kazi yangu ya filamu na nipo kwenye tasnia kwa miaka 17 na maisha yangu nayafanya ya kawaida tu wala sipendi kujikweza sana.
Kwa staili hiyo ningetumia nguvu za giza ningekuwa tajiri namba moja  hapa nchini maana siri ya kazi yoyote ni kuiheshimu na kujibidiisha. ELIZABETH MICHAEL ‘LULU’: Tasnia yetu ya filamu naona kama hatuangalii mbali maana kwa wenzetu wanashindana kikazi na si uchawi kama huku wanaofikiria kuwashusha wenzao kisa wanaona wanafanya vyema, mimi ninachoweza kusema watu wafanye kazi na wasibaki kuangalia nani anafanya nini na kumfanyia mambo kama hayo yasiojenga maisha.
RUTH SUKA ‘MAINDA’: Mimi sijui sana kama kuna watu wanafanya ushirikina. Ninachowaomba wamtegemee sana Mungu kwani ninachoamini mimi kila kitu kipo kwa makusudi ya Mungu. Kama ukimroga mwenzio ili ashuke basi hata wewe huwezi kufika mbali.
JACQUELINE PENTZEL ‘JACK CHUZ’: Kweli mimi ninaumizwa sana na watu wanaotumia uchawi kuzima nyota yangu kwa sababu kweli wapo wanaofanya hivyo tunawaona hata huko lokesheni wanakamatwa na hirizi.
Wengine wanakutwa na matunguri ila mwisho wa siku naomba wajue kuwa nyota na mafanikio ya mtu huletwa na Mungu na kujibidisha katika kazi hivyo ninachoweza kuwashauri watu kama hao waachane na imani za kishirikina.
SALUM HAJI ‘MBOTO’: Mimi ninachojua watu wanatengeneza muvi kupitia migongo ya wenzao, unakuta mtu anatengeneza sinema lakini anajua kabisa bila kumchezesha fulani hawezi kuuza hivyo anatumia nyota ya mwenzake kuuza filamu yake.
AUNT EZEKIEL: Siamini sana katika kurogana ila wanotumia njia hizo siamini kama wanafanikiwa kiasi hicho maana uigizaji ni kipaji kutoka kwa Mungu na hakuna awezae kushusha kipaji hicho ila najua uchawi upo na watu wanatumia uchawi kwenye mambo yao.
STEVE NYERERE: Uchawi haupo kwenye filamu tu hayo yapo hata kwenye siasa. Watu kibao wanatembelea nyota za watu. Wapo wanaoshinda kwa waganga, tunawajua ila cha msingi wafahamu kuwa hata ukimfanyia mtu kitu gani huwezi kuwa staa.
SALOME NDUMBAGWE MISAYO ‘THEA’: Mimi ninaona kama chalenji tu na kinyongo, maana wengi wanaotumia nguvu za giza hawachukui muda mrefu wanashuka wao. Ninachoona mimi waachane na nguvu za giza wamtegemee Mungu.
Baadhi ya waigizaji wengine waliowahi kurogwa na wenzao ni pamoja na Wema Sepetu, Blandina Chagula ‘Johari’, Nuru Nassor ‘Nora’ na wengineo.

CREDIT: GPL
Share:

Popular Posts

Copyright © ZINDUNA | Powered by Blogger